Posts

Ulezi Bora Wa Vifaranga huleta Matokeo Bora Kwenye Mradi wa Kuku!!

Image
Malezi bora ya vifaranga ni muhimu katika ufugaji wa kuku kwa sababu vifaranga hawana uwezo wa kustahimili mazingira wakiwa wenyewe mara wanapoanguliwa.Ukosefu wa malezi bora husababisha vifaranga kuwa dhaifu,kufa kwa wingi na hivyo kupunguza idadi ya kuku wa baadaye. Malezi ya vifaranga yanaweza kufanyika kwa kutumia kuku walezi au kutumia vifaa maalum. KULEA VIFARANGA KWA KUTUMIA KUKU MLEZI Vifaranga wanaweza kulelewa na mama yao au kuku mlezi. Endapo kuku wengi wametotoa vifaranga kwa wakati mmoja, achaguliwe kuku mlezi aliye na uwezo wa kulea vifaranga wengi kati ya waliototoa aendelee kulea na wengine waliototoa waachwe huru ili warudi kwenye mzunguko wa kutaga. Kuku mmoja anaweza kulea vifaranga 20 hadi 25. Mfugaji wa kuku,pamoja na kanuni nyingine, anapaswa kuzingatia yafuatayo:-  • Kuku anayelea vifaranga atengewe chumba maalumu, apewe maji ya kutosha na chakula chenye virutubisho muhimu,  • Vifaranga wasiachiwe kutoka nje hadi watakapofika umri wa wiki ...

Bora Kinga Kwa Kuku Kuliko Tiba!!!Usithubutu kusubiri Tiba.

Image
Kinga ni bora zaidi kwani ndio namna pekeee ya kuweza kuwaokoa kuku wako kwasababu magonjwa mengi hayana tiba hivyo ili kwenda sawa na kunufaika na mradi wako basi fuata ratiba hii ya chanjo kwa kuku wako!!! 1. SIKU 1. Baada ya vifaranga kutotoreshwa wenye siku moja,vifranga wapewe glucose kwa muda wa masaa 2.Glucose huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga hawa.baada ya hapo vifaranga wapewe vitamin mfano ni CHAMPRIX.Pia hii huchanganywa na maji.vifaranga wawe katika eneo lenye joto na safi. Baada ya hapo siku ya pili na kuendelea vifanga wapewe OTC plus(kijiko kimoja cha chai katika lita 5 za maji safi,pia changanya vitamin. Chanjo-Marek´s 2. SIKU YA 7 . vifaranga wapatiwe chanjo ya NEWCASTLE (KIDELI).chanjo hii huchanganywa na maji safi katika eneo lenye kivuli kasha kupewa vifaranga kwa muda wa masaa mawili kisha toa maji hayo na kuyamwaga mbali na eneo ambalo kuku wengine wanaweza kuyafikia,au kuyachimbia.baada ya hapo vifaranga wapewe maji yenye vitamin. ...