Posts

Showing posts from April 16, 2017

Darasa Kiganjani.........Njia tofauti za kufuga kuku. Faida zake Na Hasara Zake

Image
Mambo yanayomfanya mfugaji kuamua atumie njia fulani ya kufuga ni pamoja na uwezo wa kugharamia shughuli ya ufugaji wa kuku na ukubwa wa eneo alilonalo la kufugia. Katika sehemu hii utajifunza njia tatu za kufuga kuku ambazo ni:  1. Kufuga huria Kuku huachwa wenyewe kujitafutia chakula na maji. Njia hii inatumika zaidi kufuga kuku wa kienyeji. Mara chache sana mfugaji huwapatia kuku chakula cha ziada. Kwa ufugaji huu lazima kuwe na eneo kubwa la kutosha kuku kuzunguka na kutafuta chakula. Kuku hulala eneo lisilo rasmi kama vile jikoni, kwenye kiambata n.k. Faida zake  • Ni njia rahisi ya kufuga.  • Gharama yake pia ni ndogo.  • Kuku wanapata mazoezi ya kutosha.  • Kuku wanapata chakula mchanganyiko ambacho kinafaa kiafya.  Hasara zake  • Kuku huwa hatarini kuibiwa au kudhurika na wanyama wakali na hali mbaya ya hewa. • Ukuaji wa kuku ni hafifu, hufikia uzito wa kilo 1.2 baada ya mwaka. • Huharibu mazingira kama kula na mime...

Darasa Kiganjani-------Aina ya chanjo Kwa Kuku na Namna ya Kuchanja!!!

Je, una ufahamu kuwa chanjo ni kwa ajili ya kuzuia magonjwa mbalimbali yasiwadhuru kuku wako hivyo hupewa kwa kuku Wenye afya tu ambao sio wagonjwa? Na kuwa Chanjo zipo za aina kuu 2? Basi twende Pamoja!! Aina za Chanjo 1.Chanjo zilizo hai /live Virus vaccines Hizi ni chanjo zenye virusi Hai kwa ajili ya kinga dhidi ya ugonjwa fulani na ni lazima vifike mwilini vikiwa hivyo hivyo hai. *Sifa*kuu ya chanjo hizi ni kuwa kinga yake hukaa kwa muda mfupi mwilini na ndizo chanjo za awali mfano ni chanjo ya Newcastle na Gumboro. 2.Chanjo zisizo na uhai dead vaccines Hizi ni chanjo zenye virusi visivyo na uhai /vimekufa. *Aina za Chanjo kulingana na umri wa kuku* *Siku ya 1*: MAREK'S /MAHEPE. Chanjo hii hupewa kifaranga wa siku 1mara tu ya kuanguliwa na kinga hudumu kwa maisha yake yote, mara nyingi hutolewa hatchery kwenye makampuni yanayototolesha vifaranga ingawa baadhi ya makampuni hudanganya wafugaji kuwa wamechanjwa wakati hawakuchanjwa ila kwa kujiridhisha zaidi ...

Darasa Kiganjani--- MAZOEA YANAYOWAGHARIMU WAFUGAJI KUKU

Kuna baadhi ya wafugaji huwa wanafuga kwa kutegemea uzoefu walionao katika ufugaji bila ya kujali kuwa kuna mabadiliko kila siku katika sekta ya mifugo, wengi wao huwa wanatatua kesi mbalimbali zinazotokea katika ufugaji kwa kutumia uzoefu hali ambayo inawasababishia kupata hasara kubwa isiyo ya lazima. Yafuatayo ni baadhi ya mazoea yanayowagharimu wafugaji:- 1. KUINGIZA VIFARANGA BILA MAANDALIZI SAHIHI Wengi wa wafugaji huwa wanaingiza vifaranga pasipo kufuata utaratibu wa kitaalam katika kuandaa banda pamoja na maandalizi ya kupokea vifaranga. Na kama atabahatika kufanya usafi basi atafanya juujuu tu hali ambayo inasababisha banda kuhifadhi vimelea vingi vya magonjwa na kupelekea kuku kuugua na kufa kuanzia wanaingia hadi kufikia kuuzwa, na hatimaye mfugaji hupata hasara kwani hutumia pesa nyingi kwenye madawa kwa kutibu na pesa nyingi kwenye chakula kwa kuchelewa kukua kutokana na kuumwa. 2. KULISHA BILA KUFUATA MAELEKEZO SAHIHI Kila aina ya kuku wanautaratibu wa ulishw...