Posts

Showing posts with the label Quarter Acre Poultry Farm

Darasa Kiganjani.........Njia tofauti za kufuga kuku. Faida zake Na Hasara Zake

Image
Mambo yanayomfanya mfugaji kuamua atumie njia fulani ya kufuga ni pamoja na uwezo wa kugharamia shughuli ya ufugaji wa kuku na ukubwa wa eneo alilonalo la kufugia. Katika sehemu hii utajifunza njia tatu za kufuga kuku ambazo ni:  1. Kufuga huria Kuku huachwa wenyewe kujitafutia chakula na maji. Njia hii inatumika zaidi kufuga kuku wa kienyeji. Mara chache sana mfugaji huwapatia kuku chakula cha ziada. Kwa ufugaji huu lazima kuwe na eneo kubwa la kutosha kuku kuzunguka na kutafuta chakula. Kuku hulala eneo lisilo rasmi kama vile jikoni, kwenye kiambata n.k. Faida zake  • Ni njia rahisi ya kufuga.  • Gharama yake pia ni ndogo.  • Kuku wanapata mazoezi ya kutosha.  • Kuku wanapata chakula mchanganyiko ambacho kinafaa kiafya.  Hasara zake  • Kuku huwa hatarini kuibiwa au kudhurika na wanyama wakali na hali mbaya ya hewa. • Ukuaji wa kuku ni hafifu, hufikia uzito wa kilo 1.2 baada ya mwaka. • Huharibu mazingira kama kula na mime...

Darasa Kiganjani-------Aina ya chanjo Kwa Kuku na Namna ya Kuchanja!!!

Je, una ufahamu kuwa chanjo ni kwa ajili ya kuzuia magonjwa mbalimbali yasiwadhuru kuku wako hivyo hupewa kwa kuku Wenye afya tu ambao sio wagonjwa? Na kuwa Chanjo zipo za aina kuu 2? Basi twende Pamoja!! Aina za Chanjo 1.Chanjo zilizo hai /live Virus vaccines Hizi ni chanjo zenye virusi Hai kwa ajili ya kinga dhidi ya ugonjwa fulani na ni lazima vifike mwilini vikiwa hivyo hivyo hai. *Sifa*kuu ya chanjo hizi ni kuwa kinga yake hukaa kwa muda mfupi mwilini na ndizo chanjo za awali mfano ni chanjo ya Newcastle na Gumboro. 2.Chanjo zisizo na uhai dead vaccines Hizi ni chanjo zenye virusi visivyo na uhai /vimekufa. *Aina za Chanjo kulingana na umri wa kuku* *Siku ya 1*: MAREK'S /MAHEPE. Chanjo hii hupewa kifaranga wa siku 1mara tu ya kuanguliwa na kinga hudumu kwa maisha yake yote, mara nyingi hutolewa hatchery kwenye makampuni yanayototolesha vifaranga ingawa baadhi ya makampuni hudanganya wafugaji kuwa wamechanjwa wakati hawakuchanjwa ila kwa kujiridhisha zaidi ...

Darasa Kiganjani--- MAZOEA YANAYOWAGHARIMU WAFUGAJI KUKU

Kuna baadhi ya wafugaji huwa wanafuga kwa kutegemea uzoefu walionao katika ufugaji bila ya kujali kuwa kuna mabadiliko kila siku katika sekta ya mifugo, wengi wao huwa wanatatua kesi mbalimbali zinazotokea katika ufugaji kwa kutumia uzoefu hali ambayo inawasababishia kupata hasara kubwa isiyo ya lazima. Yafuatayo ni baadhi ya mazoea yanayowagharimu wafugaji:- 1. KUINGIZA VIFARANGA BILA MAANDALIZI SAHIHI Wengi wa wafugaji huwa wanaingiza vifaranga pasipo kufuata utaratibu wa kitaalam katika kuandaa banda pamoja na maandalizi ya kupokea vifaranga. Na kama atabahatika kufanya usafi basi atafanya juujuu tu hali ambayo inasababisha banda kuhifadhi vimelea vingi vya magonjwa na kupelekea kuku kuugua na kufa kuanzia wanaingia hadi kufikia kuuzwa, na hatimaye mfugaji hupata hasara kwani hutumia pesa nyingi kwenye madawa kwa kutibu na pesa nyingi kwenye chakula kwa kuchelewa kukua kutokana na kuumwa. 2. KULISHA BILA KUFUATA MAELEKEZO SAHIHI Kila aina ya kuku wanautaratibu wa ulishw...

Ulezi Bora Wa Vifaranga huleta Matokeo Bora Kwenye Mradi wa Kuku!!

Image
Malezi bora ya vifaranga ni muhimu katika ufugaji wa kuku kwa sababu vifaranga hawana uwezo wa kustahimili mazingira wakiwa wenyewe mara wanapoanguliwa.Ukosefu wa malezi bora husababisha vifaranga kuwa dhaifu,kufa kwa wingi na hivyo kupunguza idadi ya kuku wa baadaye. Malezi ya vifaranga yanaweza kufanyika kwa kutumia kuku walezi au kutumia vifaa maalum. KULEA VIFARANGA KWA KUTUMIA KUKU MLEZI Vifaranga wanaweza kulelewa na mama yao au kuku mlezi. Endapo kuku wengi wametotoa vifaranga kwa wakati mmoja, achaguliwe kuku mlezi aliye na uwezo wa kulea vifaranga wengi kati ya waliototoa aendelee kulea na wengine waliototoa waachwe huru ili warudi kwenye mzunguko wa kutaga. Kuku mmoja anaweza kulea vifaranga 20 hadi 25. Mfugaji wa kuku,pamoja na kanuni nyingine, anapaswa kuzingatia yafuatayo:-  • Kuku anayelea vifaranga atengewe chumba maalumu, apewe maji ya kutosha na chakula chenye virutubisho muhimu,  • Vifaranga wasiachiwe kutoka nje hadi watakapofika umri wa wiki ...

Bora Kinga Kwa Kuku Kuliko Tiba!!!Usithubutu kusubiri Tiba.

Image
Kinga ni bora zaidi kwani ndio namna pekeee ya kuweza kuwaokoa kuku wako kwasababu magonjwa mengi hayana tiba hivyo ili kwenda sawa na kunufaika na mradi wako basi fuata ratiba hii ya chanjo kwa kuku wako!!! 1. SIKU 1. Baada ya vifaranga kutotoreshwa wenye siku moja,vifranga wapewe glucose kwa muda wa masaa 2.Glucose huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga hawa.baada ya hapo vifaranga wapewe vitamin mfano ni CHAMPRIX.Pia hii huchanganywa na maji.vifaranga wawe katika eneo lenye joto na safi. Baada ya hapo siku ya pili na kuendelea vifanga wapewe OTC plus(kijiko kimoja cha chai katika lita 5 za maji safi,pia changanya vitamin. Chanjo-Marek´s 2. SIKU YA 7 . vifaranga wapatiwe chanjo ya NEWCASTLE (KIDELI).chanjo hii huchanganywa na maji safi katika eneo lenye kivuli kasha kupewa vifaranga kwa muda wa masaa mawili kisha toa maji hayo na kuyamwaga mbali na eneo ambalo kuku wengine wanaweza kuyafikia,au kuyachimbia.baada ya hapo vifaranga wapewe maji yenye vitamin. ...

Mwongozo kwa mfugaji wa kuku wa kienyeji,ila utafiti wa eneo lako ni muhimu sana!!

Pengine umekuwa ukiwaza sana nini ufanye ili uweze kufanikiwa na kuondokana na adha za umaskini. Yako mambo mengi ya kufanya mimi nataka kukufungua macho kwa jambo moja tu tena kwa uchache. Jambo hili anaweza kulifanya mwenye mtaji mkubwa au mdogo. Somo langu ni dogo lakini naamini wapo watakaopata mafanikio makubwa sana. Sasa kuwa makini zaidi. Unaweza kuanza kwa mtaji wa Mil.1 mpaka laki tano au hata chini ya hapo. Mfano. Unaweza kutumia Tsh 250,000 kununua kuku 25 kwa bei ya Tsh 10,000 kwa kuku mmoja (kadirio la juu) Majogoo watakuwa 5 kwa uwiano wa 1:4 .  Hii ina maana kuwa wakishaanza kutaga utakuwa na vifaranga 20 x 10 = 200 Watunze vizuri. Wale vifaranga tunakadiria kuwa makoo(majike) watakuwa 150 ambao ndani ya miezi 6-7 au zaidi nao wataanza kutaga. Utakuwa na kuku 200 + 25 =225 ndani ya miezi 14. Miezi 7 inayofuata 225 - (majogoo 55) = 170 Hii ina maana kuwa 170 x 10= 1,700.  hayo niliyotoa ni makadirio ya chini sana hivyo mpaka mwisho wa miezi 24(miak...

Mchango wa Mazingira Kwa Ulaji wa Kuku!!

Image
Kuna sababu mbalimbali zinazoathiri ulaji wa kuku, athari hizo zinaweza zikamfanya kuku ale sana au asile kabisa. Zifuatazo ni sababu za kimazingira zinazoathiri ulaji wa kuku:- JOTO Ulaji wa chakula hupungua kadri joto la mazingira linavyoongezeka, kwan kama tujuavyo zoezi la umeng'enyaji wa chakula huongeza joto la mwili, na joto la mwili halitakiwi kupanda wala kupungua, hivyo basi ubongo unamuamuru kuku asile ili kudhibiti joto la mwili lisipande. Angalizo ni kwamba mfugaji anatakiwa achunge hali ya joto la banda, kwan hata akizidisha balbu au banda likikosa hewa ya kutosha pia inaweza kusababisha joto la mazingira kuongezeka na kupelekea kuku kukosa hamu ya kula hali amabayo itawafanya kuku wadumae.  BARIDI Kipindi cha baridi kuku wanakula sana kwa sababu ubongo unamuamuru kuku ale sana kwa kuwa umeng'enyaji unatakiwa uwe mara kwa mara ili kudhibiti joto la mwili lisishuke.  Msongo Banda likiwa chafu, au lipo sehemu yenye kelele za mara kwa ma...

Ushauri Kwa Mfugaji Wa Kuku Mpya

Image
Hii ni kwa wote, wafugaji na wanaotaka kuanza kufuga. Unapotaka kuanza ufugaji unatakiwa uanze na ufugaji mdogo hatakama una mtaji mkubwa. Kwa kufanya hivi itakusaidia kupata uzoefu katika nyajna zifuatazo: UTUNZAJI Kwa kuanza na kiasi kidogo itakusaidia kujua ni ukubwa gani unafaa kwa kuku wangapi, ukiwa na kuku wangapi utalisha chakula kiasi gani, pia utapata uzoefu wa chanjo muhimu zinazohitajika hali ambayo itakurahisishia pindi utapoanza ufugaji mkubwa. SOKO Hapa tunalenga upatikanaji wa wateja wa bidhaa zako za mifugo, itakusaidia kujua wateja waliopo wanavutiwa na bidhaa ya aina gani, kwa mfano mayai utajua wanapenda mayai ya kiini cheupe au cha njano? Kwa kufaham wanchokihitaji utajua ufanye nini ili ukidhi wanachokihitaji. CHANGAMOTO Ukianza na ufugaji mdogo pia itakusaidia kujua changamoto zilizopo kwenye ufugaji na utajifunza ni jinsi gani ya kuzitatua au kukabiliananazo kabla  ya kuanza ufugaji mkubwa.

Uchambuzi Makini wa Ugonjwa Wa MDONDO/KIDERI Kwa Kuku- NEWCASTLE DISEASE.

Image
Ni ugonjwa unaowapata jamii ya ndege ambao unasababishwa na vimelea aina ya paramyxovirus. Kuenea kwa UgonjwaUgonjwa wa Mdondo (Newcastle disease) huenea kupitia njia mbalimbali kama zifuatazo:- Mayai ya kuku aliyeugua ugonjwa wa mdondo/kideri (Newcastle disease). Kugusana na kuku mgonjwa. Kupitia maji yenye maambukizi. Wakati wa totoleshaji vifaranga. Chakula chenye maambukizi. Hewa yenye maambukizi ya ugonjwa huu. Dalili za Mdondo/Kideri (Newcastle disease) Vifo vya ghafla. 2. Kutoa udenda mdomoni. 3. Kukosa hamu ya kula. 4. Kuharisha kinyesi cheupe na kijani. 5. Kuhema kwa shida. 6. Kukakamaa viungo au kupooza hasa mabawa, shingo na miguu. 7. Kupunguza utagaji. 8. Vifo hutegemea kasi ya ugonjwa huweza kufikia hadi asilimia mia moja (100%). Namna ya kudhibiti Mdondo/Kideri (Newcastle disease) Wapewe chanjo kwa muda unaofaa (Siku ya 7 na 28, na kila baada ya miezi 3). Kuku wote walioz...

DONDOO YA KUANZA UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI KAMA MRADI

Image
MAHITAJI Kuku(tetea) 10 na Jogoo 01 Banda bora Vyombo vya chakula na maji Chakula bora Madawa na chanjo kwajili ya magonjwa Chanzo cha nishati joto na mwanga Elimu na ujuzi wa malezi bora Chombo au chumba cha kutunzia vifaranga Mayai ya kuku wa kisasa/mayai mabovu(ambayo hayakuanguliwa) Madaftari au kitabu cha kutunzia kumbukumbu KUKU 10 Wakati wa kuanza mradi wako hakikisha una kuku 10 (matetea) wenye umri sawa na hawajawai kutaga hata mara moja. Chagua kuku wenye rangi nzuri kutoka katika familia bora kutegemea malengo ya mradi wako. Mfano kama lengo lako ni kuzalisha kuku wa kienyeji kwajili ya nyama basi chagua mbegu ambayo inakuwa haraka na yenye uzito mkubwa. Au ikiwa lengo ni mayai basi ni vema kuchagua aina ya kuku yenye kukua haraka na kutaga mayai mengi. Ili kupunguza gharama za manunuzi ya kuku na hivyo kuongeza faida kwa mfugaji ni vema kununua kuku wadogo ambao wametoka tu kuachishwa kulelewa na mama zao. Kuku hawa utawapata kwa bei ya chini, tena wataf...