Bora Kinga Kwa Kuku Kuliko Tiba!!!Usithubutu kusubiri Tiba.
Kinga ni bora zaidi kwani ndio namna pekeee ya kuweza kuwaokoa kuku wako kwasababu magonjwa mengi hayana tiba hivyo ili kwenda sawa na kunufaika na mradi wako basi fuata ratiba hii ya chanjo kwa kuku wako!!!
1. SIKU 1.
Baada ya vifaranga kutotoreshwa wenye siku moja,vifranga wapewe glucose kwa muda wa masaa 2.Glucose huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga hawa.baada ya hapo vifaranga wapewe vitamin mfano ni CHAMPRIX.Pia hii huchanganywa na maji.vifaranga wawe katika eneo lenye joto na safi. Baada ya hapo siku ya pili na kuendelea vifanga wapewe OTC plus(kijiko kimoja cha chai katika lita 5 za maji safi,pia changanya vitamin.
Chanjo-Marek´s
2. SIKU YA 7 .
vifaranga wapatiwe chanjo ya NEWCASTLE (KIDELI).chanjo hii huchanganywa na maji safi katika eneo lenye kivuli kasha kupewa vifaranga kwa muda wa masaa mawili kisha toa maji hayo na kuyamwaga mbali na eneo ambalo kuku wengine wanaweza kuyafikia,au kuyachimbia.baada ya hapo vifaranga wapewe maji yenye vitamin.
3. SIKU YA 14.
Wapewe chanjo ya GUMBORO .chanjo hii pia huchanganywa katika maji na kupewe vifaranga kwa muda wa masaa mawili tu.baada ya hapo vifaranga wepewe vitamin.
4. Siku ya 21.(wiki ya tatu)
Rudia chanjo ya Newcastle
5. SIKU 28(mwezi)
Rudia chanjo ya GUMBORO
6. SIKU 35(mwezi 1 na wiki 1)
Kipindi hiki kuku wapewe vitamin ya kutosha.
7. WIKI YA 6-8
KUKU wapatiwe kinga ya ndui (fowl pox).kinga hii sio rahisi kwa mfugaji asie na utaalam kuwapa kuku,tafta mtaalum kwa kazi hii au upate maeleze ya jinsi ya kuweka kinga hii.
8. WIKI YA 8
Kuku wapatiwe dawa ya minyoo na baada ya hapo unaweza kurudia chanjo ya Newcastle
Comments