MAGONJWA YA KUKU
Virus vinavyosababisha ugonjwa huu huenezwa kwa hewa
Dalili
Kuhalisha choo cha kijani na njano
Kukohoa na kupumua kwa shida
Kupinda shingo kwa nyuma
Kuficha kichwa katikati ya miguu
Kukosa hamu ya kula na kunywa
Idadi kubwa ya vifo hadi 90%
Kinga
Chanjo (New Castle vaccine) kwa mpango wa siku 3, wiki 3, miezi 3
Epuka kuingiza kuku wageni
Choma au fukie mizoga ya kuku waliokufa kwa ugonjwa
Zingatia usafi wa mazingira
Virus huambukizwa kupitia jeraha au mbu
Dalili
Vidonda vyenye utando wa kahawia/purple kwenye sehemu zinazoonekana
Kukosa hamu ya kula
Vifo vingi
Kinga
Chanja vifaranga wanapofikia mwezi 1-2 kwa kutumia chanjo ya Fowl pox vaccine
Epuka kuingiza kuku wageni
Zingatia usafi wa mazingira
HOMA YA MATUMBO/FOWL TYPHOID
Kuharisha kinyesi cha kijani na nyeupe
Kuku hukosa hamu ya kula
Kuku hukonda
Vifo hutokea kidogo kidogo kwa muda mrefu
Kinyeshi hushikamana na manyoya
Tiba
Dawa aina ya antibiotic, sulfa na vitamini
Kinga
Usafi
Fukia mizoga
Usiingize kuku wageni
Chinja kuku wote mara ugonjwa huu ukiingia na safisha banda, pia pumzika kufuga kwa miezi
MAFUA YA KUKU/INFECTIOUS CORYZA
Hutokana na bakitelia na hushambulia hasa kuku wakubwa
Dalili
Kuvimba uso
Kamasizilizochanganyikana na usaha unaonuka
Macho huvimba na kutoa machozi na pengine upofu
Hukosa hamu ya kula
Mbawa huchafuka na kutoa harufu mbaya
Tiba
Dawa za Antibiotic, sulfa na vitamini
KUHALISHA DAMU/COCCIDIOSIS
Husababishwa na vijidudu vya Protozoa
Dalili
Kuharisha damu
Manyoya husimama
Hulala na kukosa hamu ya kula
MINYOO
Dalili
Kunya minyoo
Hukosa hamu ya kula
Hukonda au kudumaa
Wakati mwingine hukohoa
Tiba
Dawa ya minyoo/Pipeazine citrate kila baada ya miezi mitatu
WADUDU
Viroboto, chawa, utitiri
Dalili
Kujikuna na kujikung'uta
Manyoya kuwa hafifu
Rangi ya upanga kuwa hafifu
Ngozi kuwa nene, ngumu na yenye magamba yanayodondoka kama unga
Kuzuia
Ziba mipasuko sakafuni na kwenye kuta za banda
Fagia banda mara mbili kwa wiki
Nyunyiza majivu au chokaa mara moja kwa wiki mara baada ya kufagia
Choma masalia ya mayai yaliyoanguliwa
Nyunyiza dawa kwenye viota
Weka maranda, majani makavu, makapi ya mpunga ya kutosha sakafuni ndani ya banda la kuku
Fuata kanuni za chanjo
Tenga kuku wagonjwa wakae mbali na kuku wazima
UPUNGUFU WA VIINI LISHE KWENYE CHAKULA KWA KUKU
Dalili
Kuku hupungua damu, uzito na kudumaa
Mifupa huwa laini na kutokuwa imara
Hutaga mayai yenye gamba laini na madogo
Huwa na manyoya dhaifu
Comments