MAGONJWA YA KUKU



Mdondo/New castle


Virus vinavyosababisha ugonjwa huu huenezwa kwa hewa
Dalili

Kuhalisha choo cha kijani na njano

Kukohoa na kupumua kwa shida
Kupinda shingo kwa nyuma
Kuficha kichwa katikati ya miguu
Kukosa hamu ya kula na kunywa
Idadi kubwa ya vifo hadi 90%
Kinga

Chanjo (New Castle vaccine) kwa mpango wa siku 3, wiki 3, miezi 3
Epuka kuingiza kuku wageni
Choma au fukie mizoga ya kuku waliokufa kwa ugonjwa
Zingatia usafi wa mazingira

NDUI YA KUKU/ FOWL POX


Virus huambukizwa kupitia jeraha au mbu
Dalili

Vidonda vyenye utando wa kahawia/purple kwenye sehemu zinazoonekana
Kukosa hamu ya kula
Vifo vingi
Kinga

Chanja vifaranga wanapofikia mwezi 1-2 kwa kutumia chanjo ya Fowl pox vaccine
Epuka kuingiza kuku wageni
Zingatia usafi wa mazingira

HOMA YA MATUMBO/FOWL TYPHOID

Kuharisha kinyesi cha kijani na nyeupe
Kuku hukosa hamu ya kula
Kuku hukonda
Vifo hutokea kidogo kidogo kwa muda mrefu
Kinyeshi hushikamana na manyoya
Tiba

Dawa aina ya antibiotic, sulfa na vitamini
Kinga
Usafi

Fukia mizoga
Usiingize kuku wageni
Chinja kuku wote mara ugonjwa huu ukiingia na safisha banda, pia pumzika kufuga kwa miezi 

MAFUA YA KUKU/INFECTIOUS CORYZA

Hutokana na bakitelia na hushambulia hasa kuku wakubwa
Dalili

Kuvimba uso
Kamasizilizochanganyikana na usaha unaonuka
Macho huvimba na kutoa machozi na pengine upofu
Hukosa hamu ya kula
Mbawa huchafuka na kutoa harufu mbaya
Tiba

Dawa za Antibiotic, sulfa na vitamini

KUHALISHA DAMU/COCCIDIOSIS

Husababishwa na vijidudu vya Protozoa
Dalili

Kuharisha damu
Manyoya husimama
Hulala na kukosa hamu ya kula

MINYOO
Dalili

Kunya minyoo
Hukosa hamu ya kula
Hukonda au kudumaa
Wakati mwingine hukohoa
Tiba
Dawa ya minyoo/Pipeazine citrate kila baada ya miezi mitatu
WADUDU

Viroboto, chawa, utitiri
Dalili

Kujikuna na kujikung'uta
Manyoya kuwa hafifu
Rangi ya upanga kuwa hafifu
Ngozi kuwa nene, ngumu na yenye magamba yanayodondoka kama unga
Kuzuia
Ziba mipasuko sakafuni na kwenye kuta za banda
Fagia banda mara mbili kwa wiki
Nyunyiza majivu au chokaa mara moja kwa wiki mara baada ya kufagia
Choma masalia ya mayai yaliyoanguliwa
Nyunyiza dawa kwenye viota
Weka maranda, majani makavu, makapi ya mpunga ya kutosha sakafuni ndani ya banda la kuku
Fuata kanuni za chanjo
Tenga kuku wagonjwa wakae mbali na kuku wazima

UPUNGUFU WA VIINI LISHE KWENYE CHAKULA KWA KUKU
Dalili

Kuku hupungua damu, uzito na kudumaa
Mifupa huwa laini na kutokuwa imara
Hutaga mayai yenye gamba laini na madogo
Huwa na manyoya dhaifu

Comments

Popular posts from this blog

Darasa Kiganjani-------Aina ya chanjo Kwa Kuku na Namna ya Kuchanja!!!

Ufugaji Wa kuku wa Kienyeji Kitaalamu-Mambo (6) ya Kuzingatia

Uchambuzi Makini wa Ugonjwa Wa MDONDO/KIDERI Kwa Kuku- NEWCASTLE DISEASE.